TANGAZO

TANGAZO

IFIKAPO 2027, MBOGWE IWE WILAYA YA KIHISTORIA DUNIANI NA SIO TZ PEKEE – MBUNGE MAGANGA



Mbunge wa Jimbo la Mbogwe Mkoani Geita, Mhe. Necodemus Maganga ameipongeza Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa Kuipa Wilaya ya Mbogwe Mkoa wa Kimadini.



Maganga amemshukuru Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati Dkt. Dotto Biteko, ambapo amesema kabla ya Kuteuliwa na Rais Mhe. Dkt Samia na kuhamishwa Wizara hiyo, alifanya jitihada kubwa mpaka kufanikisha swala hilo.

"Zamani ilikuwa shida sana, kufikisah mzigo wako 'Plant' mpaka uende Geita, na gharama za kwenda na kurudi lazima utumie mafuta zaidi ya lita 40, Kwa maana hiyo kupitia Waziri wa Madini wa nyumbani, nikajenga hoja Bungeni tukapewa RMO, na sasa hivi tunavyoongea mimi ni Mbunge wa Mkoa wa Kimadini" - alisema.

‘’Nawaomba ndugu zanguni tujipe moyo siku moja tutakuwa na mkoa kamili wa mkoa wa Mbogwe, kama tulianza na mkoa wa kimadini basi yote yanawezekana kwa Imani. Na mimi nimepanga binafsi na maombi yangu Mungu anisaidie sana ifikapo mwaka 2027, Mbogwe iwe na mabadiliko makubwa sana, Mungu akinijalia mpaka mwaka 2027 Mbogwe uwe ni mji wa kihistoria, iwe wilaya inayojulikana duniani yaani sio Tanzania tu, nataka Mbogwe ijulikane duniani, kwa hiyo wajumbe wangu naomba muwe mabalozi wazuri’’ Alisema Mbunge Maganga

Hayo yamejili leo Januari 02 2024 katika hafla ya kuukaribisha Mwaka mpya 2024, iliyofanyika katika Viwanja vya Maganga Stadium Masumbwe mkoani Geita.


Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati Dkt. Dotto Biteko katika hafla hiyo ya kuukaribisha mwaka 2024, amewataka watanzania kudumisha Umoja na mshikamano ili kuepuka chuki zinazoenezwa na watu wenye nia ovu zinazoweza kuvuruga amani hasa kulelekea kipindi cha Uchaguzi.

‘’Watu wa Mbogwe, tunaposherehekea mwaka 2024, nitoe wito nilioutoa kwa watu wa Bukombe kwa sababu nyinyi ni watu wa jamii moja ‘’Tuvumiliane’’ mwaka 2024 fanya kazi moja ya kumfanya mtu mmoja kuwa na furaha katika Maisha yake, kama kuna mtu amekukosea mwaka 2024 fanya kazi ya kumsamehe, kama kuna mtu amekutendea wema fanya kazi ya kumshukuru, kuwa na ibada ya kutenda wema kwa jirani yako, umpende kama unavojipenda wewe mtoto wa mwenzio mlee kama wa kwako, ukiona mwenzio ana tatizo, likuhusu na likuume kama tatizo lako, mkifanya hivyo mtafanya ibada iliyo njema, na mtaifanya kuwa Mbogwe ya watu wanaothaminiana na kupendana, mkifanya hivyo maendeleo mtayaona’’ Alisema

‘’Rais wetu Dkt Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa ya kuwaunganisha watanzania, kwa vyama na dini na makabila mbalimbali, anataka wote tuimbe kama watanzania wa kundi moja, na sisi wasaidizi wake tumebeba ujumbe wa Dkt. Samia Suluhu Hassan’’

‘’Jamani Watanzania Rais tulie nae amewaweka Watanzania kwenye Daraja linalofanana amesikiliza malalamiko yao, wa vyama vya upinzani walivyolalamika akawaita, akasema nawafungulieni nendeni mkafanye mikutano mueleze sera zenu, wamekuja kwenu n ahata hapa wamekuja tena kwa vyombo tofauti tofauti, wamekuja kwa magari wamekuja kwa helkopta, wamepewa fersa hiyo na serikali yetu ya kuwasaidia watanzania waweze kuzungumza yale wanayoona yanawafaa kwa maslahi ya nchi yetu, amefanya hivyo ili kujenga mshikamano na umoja kwa Watanzania’’

‘’Tutakuwa na uchaguzi mwaka huu wa serikali za mitaa kama uchaguzi huo, tuutumie kutafuta viongozi walio bora, kama kuna kiongozi anafanya kazi nzuri kama Maganga kwenye mtaa wako, mumuunge mkono mumchague, na mumpe nafasi ya kuongoza tena, kama kuna kiongozi mnaona anaweza kurekebishwa, mrekebisheni hapa sasa ivi mpaka wakati wa Uchaguzi na mumpe nafasi ya kuongoza tena’’

‘’Utakuja uchaguzi utahusisha vyama vingine vya upinzani na chama tawala kamwe watu wa Mbogwe msigawanyike kwa kutukanana kwa sababu tu ya uchaguzi, kwa sababu baada ya uchaguzi kutakuwa na maisha yanaendelea’’

‘’Muutumie huu uchaguzi kuzungumza matatizo yenu, shida yam aji, Barabara, umeme, shida ya Watoto wetu kuwa na mahali pa kusomea, mzungumze yale yanayowaunganisha kama wana-Mbogwe na msiruhusu mtu yoyote kuja kuwagawanya na kuwafundisha chuki katikati yenu’’ Alisema Naibu Waziri mkuu Doto Biteko alipokuwa akizungumza na wakazi wa Mbogwe katika Hafla hiyo ya kuukaribisha mwaka 2024


Mbunge wa Jimbo la Mbogwe Mkoani Geita, Mhe. Necodemus Maganga akizungumza.


Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Mbogwe wakiwa katika Hafla ya kuukaribisha mwaka 2024.

Post a Comment

0 Comments